Wednesday, 28 January 2015

KWA HALI HII, MUHIMU SANA KWA UKAWA KUANZISHA KIKOSI MAALUM CHA AMANI, ULINZI NA USALAMA WA UKAWA......


    Wadau wa fikra pevu na wachambuzi wa mwenendo wa kisiasa TZ, hali hii ya uonevu na unyanyasaji wa kisiasa inatisha, kinyume na Demokrasia, Amani na Utilivu ambavyo ndio msingi wa ustawi wa Jamii yoyote.

    Kwa yaliyomkumba Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA Prof Ibrahim H. Lipumba, ambaye ni MKiti wa CUF, chama ambacho kinatawala Z'Bar kupitia Katibu wake aliye makamo wa Rais, ni ufidhuli, uvurugaji na utokomezaji wa HAKI, DEMOKRASIA NA KUVURUGA AMAANI.

    Kuna haja ya UKAWA kufanya KIKAO cha Dharura na kuafiki mbinu bora, sahihi na za msigi kuanzisha kikosi cha AMANI, Ulinzi na Usalama cha UKAWA, ambacho ikiafikiwa kitambukike kama 'UKAWA WHITE BRIGADE-15' au kwa kifupi UWB-15); Kitakuwa Kikosi maalum CHA AMANI NA UTULIVU wa TAIFA JIPYA, na hasa Viongozi wake.

    Tafsiri: Dhana 'WHITE' = Amani na Utulivu [Kusimamia HAKI, AMANI NA UTULIVU hadi inapotokea hatari NDIO wachukue action kali na stahiki kulinda], na namba -15,= yaani Mwaka 2015, mwaka ambao UKAWA inaelekea kulikomboa Taifa na kuzaa Taifa jipa la Tanganyika, kutoka ktk mikono ya utawala wa mabeberu na ma-nazi meusi CCM. Wayafanyao watawala hawa yanajidhihirisha wazi kuvunjika kwa utawala. Huwa hatua ya kwanza za tawala zinazoanguka ni kueneza woga kwa wanaotaka kujenga fikra huru, kutisha watu na kuzuia hisia za fikra mpya, kuvuruga kujiamini na kuchochea mgawanyiko. Ndio tunayoyaona sasa, na tutayaonana matukio mengi zaidi kwa jinsi tunavyosogea uKOMBOZI na kuchagua utawala mpya Oktoba 2015! Tusichelewe kuchukua maamuzi ya muhimu.

    Naomba kuwasilisha!

No comments:

Post a Comment