Wednesday, 3 December 2014

Wednesday, December 3, 2014

UWEZO WA VYUO VIKUU KUCHUKUA WANAFUNZI WA SAYANSI BADO CHANGAMOTO KWA TANZANIA KUTIMIZA MALENGO YA EFA

DSC_0341
Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi nchini Tanzania Mh. Dkt. Shukuru Kawambwa akifungua mkutano wa kimataifa wa kutathmini mafanikio na changamoto za utekelezaji wa malengo ya Mpango wa Kimataifa wa Elimu kwa Wote-EFA uliofanyika jijini Dar Es Salaam ambapo amesema tangu mwaka 2000 Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuelekea kutimiza malengo ya Mpango huo ikiwa ni utashi wa kisiasa na kuwajibika vikisaidiwa na kujitolea kwa wadau wa sekta ya elimu pamoja na washirika wa maendeleo.(Picha na Zainul Mzige wa MOblog).

Tanzania imekuwa moja wapo ya nchi za kutolea mfano miongoni mwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara katika kutekeleza maazimio ya mpango wa Elimu kwa wote (EFA).Akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa wadau wote wa elimu , Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi nchini Tanzania Mh. Dkt. Shukuru Kawambwa amesema Tanzania Bara na Visiwani imeweza kukaribia kufikia malengo ya mpango huo ikiwa ni pamoja na suala la wastani wa waalimu kwa wanafunzi.
Amesema kwamba kwa shule za msingi Tanzania Bara imefikia wastani wa wanafunzi 47 kwa mwalimu mmoja wakati Visiwani Zanzibar ni wastani wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 27. Mafanikio mengine yaliyopatikana chini ya mpango huo ni kuboresha wastani wa wanafunzi kwa darasa, ambapo kwa Tanzania Bara wastani umetoka kuwa wanafunzi 92 kwa darasa na sasa ni wanafunzi 65 huku Zanzibar wastani ukiwa ni wanafunzi 62 kwa darasa.
DSC_0288
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza wakati wa mkutano wa kimataifa wa kutathmini mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika kutekeleza malengo ya Mpango wa Kimataifa wa Elimu kwa Wote –EFA ulioshirikisha wadau wote wa sekta ya elimu uliofanyika jijini Dar Es Salaam. Amesema lengo kuu la mkutano huo ni kuiandaa Tanzania kuweza kushiriki kikamilifu katika mashauriano ya kiserikali baina nchi mbalimbali na kuhakikisha wadau wakuu wa elimu kitaifa wanapata taarifa juu ya mapendekezo ya agenda zitakazoanza mwaka 2015.
Awali Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues amesema ikumbukwe kwamba malengo nane (8) ya EFA yanachangia kufanikisha Malengo Makuu ya Maendeleo ya Millennia (MGDs) yaliyopitishwa mwaka 2000 kati ya nchi 189 na Taasisi za Mendeleo zinazoongoza Duniani.
Bi. Rodrigues amefafanua kuwa tunapoelekea mwaka 2015, Tanzania Bara na Visiwani zimeonyesha juhudi katika kupunguza tofauti kubwa zilizokuwepo kielimu ikiwa ni pamoja na kukabilia na changamoto zilizojitokeza na kuweza kuweka sera, mipango na utawala bora katia Nyanja za fedha , wadau, usimamizi na uwajibikaji.

BENKI YA CRDB YASAINI MKATABA WA HALI BORA ZA WAFANYAKAZI WAKE

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza wakati wa uwekaji saini wa Mkataba wa Hali Bora za Wafanyakazi na Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO) uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Dorah Ngaliga na Katibu wa Benki, John Rugambo. 
 Baadhi ya maofisa wa CRDB wakiwa katika mkutano huo.
 Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO),
Shikunzi John akizungumza katika hafla hiyo. Kulia ni
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Dorah Ngaliga, Katibu wa Benki, John Rugambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (katikati) akisaini mkataba wa hali bora za wafanyaka wa benki hiyo na Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO), Shikunzi John.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia) akisaini mkataba wa hali bora za wafanyaka na Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO), Shikunzi John (wa pili kulia).
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia) na Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO), Shikunzi John, wakibadilishana hati ya Mkataba wa Hali Bora za Wafanyakazi wa benki hiyo na TUICO jijini Dar es Salaam. 


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia) na Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO), Shikunzi John, wakibadilishana hati ya Mkataba wa Hali Bora za Wafanyakazi kati ya Chama hicho na Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.   

Na Mwandishi Wetu

BENKI ya CRDB na imetiliana saini mkataba na Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Viwanda, Huduma na Biashara (TUICO) wa kuboresha hali bora za wafanyakazi wa benki hiyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, alisema mafanikio yoyote ya kibiashara hayapatikani kama wafanyakazi ambao ndio wazalishaji hwatakuwa na mazingira yenye maslahi bora na motisha mbalimbali.

Dk. Kimei alisema nia ya CRDB ni kuboresha mahusiano kati ya mwajiri na wafanyakazi, kuboresha mazingiraya utendaji kazi ili kuchochea ufanisi, kurasimisha mahusiano kati ya benki na wafanyakazi kwa kuweka miongozo itakayosaidia kupunguza mifarakano kati ya CRDB na wafanyakazi.

“Mkataba huu ni wa miaka mitatu, utasaidia kuajiri na uthibitishwaji wa wafanyakazi kazini, kushughulikia migogoro ya kikazi, uhamisho wa viongozi wa chama cha wafanyakazi sehemu ya kazi,utaratibu wa likizo ya uzazi, likizo ya ugonjwa, ulipwaji gharama ya usafirishaji mizigo kwa wafanyakazi wanaohamishwa, mazishi ya wazazi wa wafanyakazi, bima na utoaji tuzo,”alisema  
Aidha alisema

WAJASIRIAMALI WAELEZEA WALIVYOWEZESHWA NA PROMOSHENI YA SAFARI LAGER WEZESHWA YA TBL

 Jacquline Shija Mazemle, aliyewezeshwa na TBL na kufanikiwa kuanzisha mghahawa maarufu wa FACEBOOK, ulioko karibu na Chuo Kikuu cha Kampala, Gongo la Mboto, Dar es Salaam.
Akiandaa chakula na wenzake Ramadhan Seleman kushoto na Hans Shija
 Akiwahudumia na wateja wa Facebook
 Dorren Asey aliyewezeshwa na TBL kutengeneza mikate, keki na maandazi kupitia kampuni yake ya Dee Bakery,Doreen akiandaa mikate
 Doreen akiandaa mikate
 Dorren akionyesha mashine ya zamani


 Dorren kulia na msaidizi wake Ali Chares


 Dorren Assei akionesha moja ya majiko ya kuokea mikate
 Hapa ndio Facebook
 Jacquline Shija akielezea kuhusu mafanikio yake baada ya kuwezeshwa na Safari Lager Wezeshwa

Tuesday, December 2, 2014

UZUSHI WA MBUNGE WA JIMBO LA MOROGORO MJINI KUVUNA WANACHAMA 167 KUTOKA UKAWA SIYO KWELI ILIKUWA MICHEZO YA KUIGIZA NA WALIO NUNULIWA KUFANIKISHA HAYO WAMEFUNGUKA! NA KUDAI WALIRUBUNIWA KUFANYA HIVYO NA KUTAPELIWA KIASI CHA PESA WALICHO AHIDIWA. CCM CHAFUUU!

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Kulia akimsikiliza Aliyekuwa Mwenyekiti Baraza la Vijana la Chama cha wananchi CUF Wilaya ya Morogoro Ndugu Mariam Iswili aliyeamua Kurudisha Kadi ya Cuf na Kujiunga na Chama cha Mainduzi.Katika Tukio Hilo jumla ya wanacha 167 Kutoka Vyama vya CUF CHADEMA na NCCR MAGEUZI Walirudisha kadi zao na kusema vyama hivyo havina sera Mya zaidi ya Majungu na Maneno Mengi yasiyo na Tija kwa wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Kiwa na Kadi ya Cuf aliyoiokea.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Akionyesha kazi alizokabidhiwa kuto kwa wanachama waliohama kutoka vyama vya CHADEMA  na CUF na Kuhamia CCM
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Za vyama vya chadema CUF na Nccr Mageuzi alizookea Kutoka kwa wanachama wa Vyama Hivyo na Kuamua Kujiunga na chama cha Mapinduzi .





Waliokuwa wanachama wa Ukawa wakila kiao mara baada ya Kukabidhiwa kadi za CCM

Wanafunzi Tisa (9) -Wahitimu mafunzo ya uuguzi na ukunga

Rasilimali watu ni changamoto kubwa inayoikabili sekta ya afya nchini Tanzania. Upungufu huu unaathiri mfumo wa utoaji huduma bora na kwa wakati kwa wahitaji. Upungufu wa wahudumu wa afya  wenye ujuzi unaathiri ngazi zote za huduma na hasa vijijini. Kutokana  na wauguzi wakunga kuwa kiini katika utoaji  huduma za afya   vijijini na mijini kwa ujumla,  kuna umuhimu wa  wakunga hawa kupata elimu ya ujuzi  wa kutosha ili waweze kuwafikia wahitaji zaidi ya asilimia  sabini (70%)  ya  jumla ya wananchi wanaoishi vijijini.

Katika kupambana na changamoto ya upungufu wa wahudumu wa afya hasa katika kulenga  kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua, Amref Health Africa imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha taasisi, mashirika na watu binafsi kuchangia mafunzo ya wakunga watalaam   ili waweze kutoa huduma salama, sahihi na kwa wakati ili kupunguza vifo vinavyoweza kuepukika wakati wa kujifungua.

Jumla ya Wanafunzi 121 wamehitimu mafunzo ya uuguzi ukunga ngazi ya cheti katika chuo cha Muheza School of Nursing mkoani Tanga.  Miongoni mwa wanafunzi hao 9 walikuwa wakisoma kwa udhamini wa Barclays bank kupitia kampeni ya “Stand up for African Mothers” inayoendeshwa na Shirika la afya la Amref Health Africa Tanzania.

Barclays Bank ni mshiriki mkubwa katika kampeni hii  na anatoa udhamini wa kusomesha wanafunzi  katika ngazi ya cheti na hivi leo  tumeshuhudia  wanafunzi 9 wamehitimu tayari kwa kwenda kutoa huduma katika jamii zinazowazunguka. Wahitimu hawa wanakwenda kufanya kazi maeneo ya vijijini Kama moja ya lengo na nia ya kampeni ya stand up for African mothers ambayo inalenga kupunguza vifo vya mama na mtoto hasa maeneo ya kijijini na yaliyo magumu kufikika.

Juhudi za Amref Health Africa na Barclays bank  ni endelevu  na wito unatolewa  kwa mashirika, makampuni ya umma na yale ya binafsi, pamoja na watu binafsi  kuunga mkono jitihada hizi kwa kudhamini mafunzo ya wakunga (mafunzo ya mkunga  kwa miaka miwili  yanagharimu dola 3000). Unaweza kuchangia kwa njia mbali mbali, ikiwa ni pamoja na kupitia

Bank  account at Bank M, Kisutu Branch , Akaunti Namba  0250027331
Account ya benki National Bank of Commerce (NBC), Corporate Branch, Akaunti Namba 0111030004548
Mpesa Namba 0762 22 33 48
Tigo pesa Namba 0716 032 441
Airtel money Namba 0685 506306.

Stand Up For African mothers ni kampeni ya kimataifa inayolenga kuelimisha na kutoa taarifa juu ya umuhimu na mchango wa wakunga wenye ujuzi katika kupunguza viofo vya mama na watoto wakati wa kujifungua.  Kampeni hii inayoendeshwa na Amref Health Africa inalenga kusomesha wakunga 15,000 katika nchi kumi na tatu za Africa wakati Tanzania ikitarajia kusomesha wakunga 3800.
Dr. Pius Chaya,mkuu wa kitengo cha kujenga uwezo Amref Health Africa Tanzania akimuwakilisha Mkurugenzi , Dr. Festus Ilako wakati wa mahafali Chuo hapo.
Jumla ya wanafunzi 121 waliohitimu uuguzi ngazi ya Cheti, miongoni mwao wakiwemo tisa (9) waliofadhiliwa na Barclays kupitia Stand u For African Mothers Campaign inayoendeshwa na Amref Healt.
Mkuu wa Chuo akiwa pamoja na viongozi, wakufunzi wengine katika picha ya pamoja.
Mkuu wa Chuo, Baba Askofu pamoja na viongozi wa madhehebu mengine katika picha ya pmaoja.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AFUNGUA MKUTANO WA WATAALAMU WA UGAVI JIJINI ARUSHA

Mwandishi wetu,Arusha

WIZARA ya Fedha, imeitaka Bodi ya Wataalam wa Ugavi na Manunuzi nchni  (PSPTB), kutafuta ufumbuzi wa tatizo la kufanya manunuzi bila kuzingatia thamani halisi ya fedha na kuwataka waajiri kuacha mara moja kuwaajiri watu wasio na sifa kufanya kazi hizo

Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano wa tano wa mwaka wa Siku mbili unaofanyika kwenye jengo la Mikutano la AICC jijini Arusha ambapo aliwataka Wataalamu hao kuzingatia maadili na miiko ya kazi yao.

Amesema katika bajeti ya mwaka 2014/15 serikali imetega bajeti ya Sh trilioni 20 kati ya hizo asilimia 65 hadi za 70 zinatumika kwenye manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali,hivyo taaluma hiyo kuwa na umuhimu wa kipee katika kudhibiti mapato ya serikali yasitumike vibaya.

Awali Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Sr. Dk. Hellen Bandiho, amesema kauli mbiu ya mkutano huo “Thamani halisi ya fedha za Manunuzi” ikilenga kuhakikisha serikali inapata huduma bora kulingana na fedha inazotumia ili kuinua uchumi wa nchi.

Amesema Bodi hiyo imezalisha wataalam zaidi ya 23,000 katika ngazi mbalimbali ambayo ni sawa na asilimia 47 pekee huku waajiri wengi wakiwa wamewajiri watumishi wasiosajiliwa na Bodi hiyo.
Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima akiongoza na maafisa wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) katika mkutano wa Siku mbili unaofanyika kwenye kituo cha mikutano cha AICC, jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima akisoma hotuba yake kwenye mkutano wa Siku mbili wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB)  unaofanyika kwenye kituo cha mikutano cha AICC jijini Arusha.
Baadhi ya Maafisa Ugavi na Ununuzi wakisoma nyaraka mbalimbali za mkutano huo leo jijini Arusha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB)Clemence Tesha(kulia)akimpongeza Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima kwa hotuba nzuri.
Wataalamu wa Ugavi na Ununuzi nchini wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Wazi wa Fedha

CLOUDS FM YASHEREHEKEA KUTIMIZA MIAKA 15 TANGU KUANZISHWA KWAKE.

Mmoja wa Watangazaji machachari wa Clouds FM,Adam Mchomvu akitoa muongozo mfupi kwa baadhi ya Wafanyakazi wenzake waliomzunguka,kuhusiana na ukataji na ulaji wa Ndafu kama ionekavyo pichani,wakati wa hafla ya kutimiza miaka 15 ya kituo cha redio ya Clouds FM,tangu kuanzishwa kwake nchini.Redio hiyo imejizolea umaarufu mkubwa Afrika Mashariki na Kati na Duniani kwa ujumla
 Mkurugenzi wa Uzalishaji na Vipindi Ruge Mutahaba akilishwa kipande cha Ndafu na mtangazaji wa kipindi cha XXL,Dj Fetty,huku miluzi na shangwe za hapa na pale zikiwa zimetawala mjengoni humo,Mikocheni jijini Dar
 Msanii mkongwe wa Muziki wa kizazi kipya,Prof Jay akilishwa kipande cha ndafu,wakati wa hafla ya muendelezo wa redio hiyo kutimiza miaka 15 tangu kuanzishwa kwake nchini.
 Mkuu wa Vipidi wa Clouds FM,Sebastian Maganga akishukuru jambo kwa baadhi ya Wafanyakazi wenzake mara baada ya kulishwa keki na Mtangazaji wa kipindi cha XXL,Dj Fetty.
 Dj Mkongwe ndani ya Clouds FM,Dj Venture akilishwa keki kwenye hafla hiyo ya kutimizwa miaka 15 kituo hicho maarufu cha redio hapa nchini na kwingineko.
 Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa kizazi kipya,Banana Zorro akihojiwa mambo kadhaa kuhusiana na hafla ya muendelezo wa kituo hicho cha redio kutimiza miaka 15 tangu kuanzishwa kwake nchini.
 Msanii wa zamani wa Bongofleva aliyewahi kuwa kwenye kundi la B Love M,Masiga Msigalla
 Kulikuwepo na wimbo wa kuimba pamoja
 Ndafu wa shughuli akiwa mezani
 Ndafu akitolewa nje ili aliwe vizuri
 Wadau mbalimbali pia walikuwepo.
 Shayo akihakikisha kila mmoja anapata kipande cha Ndafu
 Mkuu wa Vipindi wa Clouds FM,Sebastian Maganga akihojiwa machache na Mtangazaji wa Clouds TV,Antonia Nugaz
Kutoka  Idara ya Muziki Clouds FM,anaitwa Othman Suka na Da Husna mtangazaji wa kipindi Leo Tena
 Mrope nae akigawa vipande vya Ndafu
 Kutabasamu,kuwhatsapika pia kulikwepo mjengoni hapa
''Heee hii imetoka vizuuuriiii..''
 Adam Mchovu akiwatangazia baadhi ya wafanyakazi wenzake kuhusiana na utaraibu mzima wa kwenda kujiachia kwenye kiota cha maraha cha Escape One.
Mazungumzo ya hapa na pale ya kishosti yalinoga pia huku ndafu akiliwa taratibuu.

No comments:

Post a Comment